MKUTANO MKUBWA WA INJILI MBULU
NA HUDUMA YA KINDNESS & UMOJA WA
CPCT MBULU
Huduma ya KINDNESS ikishirikiana
na makanisa ya Kipentekoste Mbulu CPCT inaandaa mkutano mkubwa wa injili Mbulu
tarehe 02/10/2016
hadi tarehe 08/10/2016.
Kwa mjibu wa mkutano/ kikao cha
wachungaji wa makanisa ya CPCT Mbulu na Kiongozi wa huduma ya Kindness na
Mwinjilisti Ndg Msengi toka Singida, kilichofanyika tarehe 11/7/2016 na tarehe 16/08/2016
chini ya Mwenyekiti wa umoja huo wa CPCT Mbulu Mch Isaya na Mwangalizi wa
makanisa ya TAG Mbulu, pamoja na wachungaji wa umoja huo wa CPCT Mbulu toka
makanisa ya TAG, CALVARY, VICTORIUS, GRC, FPCT, EAGT na mengineyo.
Kutakuwa na Mkutano mkubwa sana
wa Mavuno katika mji wa Mbulu, pamoja na sinema pea tatu ambazo zitaonyeshwa
kila siku katika maeneo matatu tofauti.
Kabla ya mkutano wa injili,
utatanguliwa na semina elekezi ambayo itasaidia sana kwa ushuhudiaji wa Neno la
Mungu nyumba hadi nyumba ambapo wainjisti zaidi ya 30 wanategemewa kuwasili
Mbulu kwa huduma hiyo ya uinjilisti wa nyumba hadi nyumba katika mji wa Mbulu
na viunga vyake kutokana na uhitaji wa makqanisa ya CPCT Mbulu. Kila atakayefundishwa
semina elekezi atatoa sh 2000 na watoto sh 1000.
Mwisho wa mkutano kutakuwa na
ubatizo wa maji mengi kwa wote wayakaompa Yesu maisha yao.
Mungu amesema na watumishi wake
wa huduma ya Kindness na hawawezi kutulia kwa ajili yako. Yeremia 47:7b.
Unasubiri nini sasa? Usikose mkutano huo wa Baraka.
Umoja huo wa CPCT Tanzania kwa
sasa upo Vizuri. Hatua inayofuatia ni kuimarisha umoja huu wa makanisa ya CPCT
katika ngazi ya Mikoa na Wilaya hadi vijijni.
Katiba ya umoja huu ambayo kwa
sasa ndiyo inasubiriwa, itasaidia sana kuimarisha umoja wetu wa CPCT Taifa,
Mikoni hadi Wilayani.